JWTZ YAPEWA JUKUMU JIPYA LA KULINDA AMANI NCHINI KONGO

Akizungumzia hatua ya vikosi vya JWTZ kupewa jukumu jipya nchini Kongo, Msemaji wa jeshi hilo nchini, Luteni Kanali Erick Komba alisema kuwa hilo si jukumu jipya bali ni jukumu la kawaida, ambalo wanalitekeleza kulingana na maagizo ya Umoja wa Mataifa.

“Kwa wapiganaji wetu hilo sio jukumu jipya, wanatekeleza majukumu yao ya kawaida, wamekuwa kazini kila siku, hakuna siku ambayo wamepumzika, jukumu lao ni kuhakikisha vikundi vya waasi vinakwisha, sasa kila kinapoibuka na kama wanatakiwa kuwashughulikia wanatekeleza hilo, hakuna jukumu jipya hapo,” alisema Luteni Kanali Komba.

Kuhusu wanajeshi hao kurejea nchini kuanzia mwezi Aprili, alisema suala hilo ni la ndani na hawezi kulizungumzia na kwamba wakati wa kufanya hivyo ukifika atazungumza.

“Ndugu yangu suala la kurudi ama kutorudi ni la ndani, wale wako kule kwa ajili ya kulinda amani, wakati wa kulizungumzia hilo ukifika bila shaka tutafanya hivyo,” alisema.

>>Mtanzania

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger