LINEX AKANA KUWA NA UHUSIANO NA MASOGANGE ASEMA HANA HARAKA NA MAPENZI

Linex Sunday Mjeda, ambaye hivi karibuni ameonekana kwenye picha kadhaa akipoz na video Queen maarufu Tanzania, Agnes Gerald (Masogange), amekanusha kuwa na uhusiano wa mapenzi na mrembo huyo.
 
Kupitia akaunti yake ya Facebook, mkali huyo wa ‘Kimugina’ ameonesha kusikitishwa na habari iliyoandikwa na tovuti moja kuwa yeye na Agnes wako kwenye mapenzi mazito.
 
“Ni kweli watu wa blog mnapush sana kazi zetu but nimesikitishwa na habari hii iliyoandikwa na blog kadhaa mtasababisha tutashindwa ata kukaa na Dada zetu au marafiki zetu Uliza b4 Hujaandika ujinga am single na sina haraka ya kua na mpenzi.” Ameandika kwenye Facebook.
 
Wikendi hii, Linex alipost picha mbili Instagram akiwa na mrembo huyo, moja wakiwa wamepoz ufukweni, na nyingine akiwa naye katika mechi ya mpira wa kikapu kati ya timu za madirector wa video za muziki Tanzania, Adam Juma na Karaban.

>>Times 100.5 FM

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger