PNC NAYE AONDOLEWA MTANASHATI ENTERTAINMENT, SABABU HANA NIDHAMU

Siku kadhaa baada ya Janjaro kuondolewa kwenye familia ya Watanashati Entertainment, Pacras Ndaki aka PNC naye amefunguliwa ‘exit door’ na kutolewa nje ya usimamizi wa kampuni hiyo.
Akizungumza na tovuti ya Times FM, boss wa kampuni hiyo, Ostaz Juma amedai kuwa hatua hiyo imetokana na utovu wa nidhamu uliooneshwa na msanii huyo kwa kutofuata sharia za Watanashati Entertainment, ikiwa ni pamoja na kufanya shows bila kuutarifu uongozi.

‘Unajua PNC alipokuja Mtanashati aliniomba nimsimamie kazi zake kwa kutumia fedha zangu, lakini unakuta anapoenda kupiga show kadhaa hanijulishi, wakati mimi ninatumia pesa nyingi sana kumgharamikia, sasa kuna umuhimu gani wa mimi kumsimamia? Ameiambia tovuti ya Times Fm.

“Sio yeye tu, na Dogo Janja, wote hawana utovu wa nidhamu kabisa, mara kumi fedha zangu nizipeleke msikitini au kwa watoto yatima nibarikiwe kuliko kukaa na watu wasiokuwa na nidhamu.” Boss wa Watanashati ameongeza.

Tovuti ya Times Fm, ilizungumza pia na PNC ambaye licha ya kukiri kuondolewa Watanashati, alikanusha madai ya Ostaz Juma ya kuwa mtovu wa nidhamu.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger