WASANII WALIOHUDHURIA SHEREHE ZA CCM WALIPWA JUMLA YA SHILLINGI MILLION 8

Kwa mujibu kwenye taarifa iliyoandikwa kwenye mtandao wa Jamii Forums (ambayo hata hivyo haijathibitishwa binafsi na Bongo5), wasanii wa Bongo Movies waliohudhuria maadhamisho ya miaka 37 ya Chama Cha Mapinduzi, CCM wiki iliyopita, walililipwa shilingi milioni 8 jumla. Jumla ya wasanii 10 walihudhuria maadhimisho hayo na hiyo inamaanisha kuwa kama ni kweli walilipwa shilingi milioni 8, kila mmoja alipata gawio la shilingi laki 8.
0L7C0312 JB akizungumza kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya
“Habari nilizozinyaka kutoka kwa chombo cha uhakika ni kuwa wasanii wa bongo movie walilipwa Tsh. Milioni 8 kwa kuhudhuria maadhimisho ya kutimiza miaka 37 na kujiunga na chama cha mapinduzi. Aliyefanya malipo haya ni Nape Nnauye na walipewa cash nina uhakika mh. Rais hakuwa analifahamu hili,” taarifa hiyo imesema.
6
Wasanii hao ni pamoja na Jacob Stephen, Irene Uwoya, Blandina Chagula,Mboto,Single Mtambalike, Haji Adamu aka Baba Haji, Slim Omar, Wastara na wengine.
9
Sherehe hizo zilifanyika kwenye uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, ambapo wasanii hao walikabidhiwa kadi za uanachama.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger