MZEE SMALL AFARIKI DUNIA




Muigizaji mkongwe hapa nchini,said ngamba maarufu kwa jila la mzee small amefariki dunia usiku wa leo katika hospitali ya taifa muhimbili alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Akithibitisha taarifa ya kifo cha mzee small,mwanae aitwae mahmoud amesema mzee wake amefikwa na mauti hayo majira ya saa nne usiku wakati akiwa hospitalini hapo akiendelea kupatiwa matibabu.

Mipango inafanyika nyumbani kwao tabata na kadri taarifa zitakavyokuwa zikitufikia tutaendelea kujulishana.

Ni pigo lingine tena kwenye tasnia ya sanaa baada ya kuondokewa na wasanii kadhaa majuma yaliyopita.

Mdadisi wa Mambo blog imepokea taarifa hii kwa masikitiko makubwa sana na inamuombea kwa mwenyezimungu aiweke roho yake mahala pema peponi.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger