Kumbe! Siri imefichuka sababu ya malori ya mizigo na mafuta kuungua
moto baada ya jeshi la polisi mkoani hapa kuwashikilia watu sita akiwemo
dereva na utingo wa lori aina ya Scania, mali ya Kampuni ya Dandu
wakidaiwa kuchoma moto lori hilo.
Ilidaiwa kwamba jamaa hao wakazi wa Mbeya walifanya hivyo baada ya
kutaifisha mzigo wa mitumba na viatu wenye thamani ya shilingi milioni
100 waliokuwa wakiusafirisha kwenye lori hilo kwenda Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo.
Ilidaiwa kuwa wawili hao walifanya njama ya kulichoma moto lori hilo
baada ya kushusha mzigo huo na kuuhifadhi kwenye Kijiji cha Maguhani
Mufindi ili kuuuza kutokana na dereva wa lori hilo kudaiwa kodi ya
shilingi laki 4 na baba mwenye nyumba.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Ramadhan Mungi alisema watu
sita wanashikiliwa na jeshi hilo wakihusishwa na tukio hilo na kuwa
lori hilo lilikuwa na mzigo wenye thamani ya shilingi milioni 100.
Mungi alisema kuwa, polisi wakiwa doria katika maeneo ya Mafinga
wilayani Mufindi walikuta lori likiungua bila kuwepo kwa dereva wala
utingo.
Baada ya uchunguzi walimbaini dereva wa lori hilo alijulikana kwa jina moja la Elia (26) na utingo wake, Deusi (20).
Alisema kuwa watuhumiwa hao waliwasha moto lori hilo baada ya
kushusha kwa magendo mzigo huo wa mitumba kwa mtu aliyetajwa kwa jina
moja la Agrey.
Dereva
na utingo huyo walipoulizwa na gazeti hili walidai kuwa kuungua kwa
malori ya mizigo kunatokana na mbinu mpya iliyobuniwa ya kufanya hivyo
baada ya kuuza mzigo na kuwa wakati mwingine madereva hulazimika
kujikata na visu ama vitu vyenye ncha kali ili kusingizia kutekwa pindi
wanapouza mzigo yakiwemo mafuta na mizigo mingine.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment