ASTAA WASUSA 40 YA JAPANESE, SABABU HII HAPA

MWANAMUZIKI aliyefariki dunia, Amina Ngaluma maarufu kama Japanese alifikisha siku 40 tokea azikwe Jumamosi iliyopita, lakini katika kisomo kilichosomwa nyumbani kwao Kitunda, hakuna staa yoyote wa muziki wa dansi aliyehudhuria.
Mwanamuziki Amina Ngaluma enzi za uhai wake.
Japanese alifariki dunia mwezi uliopita nchini Thailand alikokuwa akifanya kazi ya muziki na katika shughuli hiyo ya wiki iliyopita, masheikh mbalimbali walihudhuria kwa kisomo kabla ya kufuturisha watu.
Kabla ya mauti kumfika, Japanese aliwahi kufanya kazi kwa kujituma katika bendi za African Revolution ‘Tam Tam’, Double M Sound na TOT, lakini katika hali ya kusikitisha hakuna hata mwanamuziki mmoja aliyehudhuria zaidi ya mumewe, Rashid Sumuni.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger