BATULI AGOMA KUFUTURISHA VIBOSILE

MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ ametamka kuwa hakubaliani kabisa na wale mastaa wenye tabia za kufuturisha watu wenye uwezo mkubwa kiuchumi.
Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’
Akizungumza na paparazi wetu, Batuli alisema anaamini kwamba twawabu nzuri zinapatikana kwa kufuturisha watu wenye mahitaji kama watoto yatima na ndiyo maana yeye amejiandaa kuwafuturisha.
“Wasanii tubadilike, tuwafuturishe watu wenye mahitaji ili kuwafanya na wao wafurahi, banafsi nitafanya hivyo mwezi huu, nitafuturu na wasiojiweza,” alisema Batuli.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger