CHEKIBUDI ADAIWA KUDHULUMU KAZI YA FILAMU YA MWANADADA

STAA wa sinema za Kibongo, Nurdin Mohammed ‘Chekibudi’ amejikuta ameingia kwenye bifu kali na mwigizaji Helen Luanda ‘Zerishi’ baada ya mwanadada huyo kumtuhumu kuwa amemdhulumu kazi yake ya filamu.Staa wa sinema za Kibongo, Nurdin Mohammed ‘Chekibudi’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Zerishi alisema aliamua kumshirikisha Chekibudi kwenye kazi yake na kukubaliana naye ampelekee filamu yake sokoni na kumlipa shilingi milioni nne baada ya filamu hiyo kuuzwa lakini kaingia mitini.
Alipotafutwa Chekibudi kuhusiana na madai hayo alikana kumdhulumu na kusema vitu vyote anavyo Zerishi isipokuwa demo anayo yeye.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger