HATIMAYE UJERUMANI ACHUKUA UBINGWA WA KOMBE LA DUNIA


Wachezaji wa Ujerumani wakishangilia baada ya kutwaa Kombe la Dunia kwa mara ya nne nchini Brazil usiku huu.
Kocha wa Ujerumani, Joachim Low akinyanyua juu Kombe la Dunia.
Mario Gotze akiifungia Ujerumani bao pekee na la ushindi dhidi ya Argentina usiku huu.
Wachezaji wa Ujerumani wakishangilia na Gotze.
Aliyekuwa mchezaji wa Barcelona, Carles Puyol (kushoto) na modo wa Brazili, Giselle baada ya kuleta Kombe la Dunia uwanjani kabla ya mechi ya fainali kati ya Argentina na Ujerumani kuanza.
Meesi na Neuer wakiwa na tuzo zao.
TIMU ya Ujerumani imetwaa Kombe la Dunia 2014 kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Argentina katika muda wa nyongeza baada ya suluhu kwenye muda wa kawaida wa dakika 90.
Bao hilo lililoipa ushindi  Ujerumani limefungwa na Mario Gotze dakika ya 113 ya mchezo na kuifanya timu hiyo kutwaa Kombe la Dunia mara ya nne baada ya mwaka 1954, 1974 na 1990.
Katika michuano hiyo, kipa wa Ujerumani, Manuel Neuer ametwaa tuzo ya kipa bora, Lionel Messi wa Argentina akitwaa tuzo ya mchezaji bora huku mshambuliaji wa Colombia, James Rodriguez akiwa ndiye mfungaji bora baada ya kutia kambani mabao sita.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger