Mfanyakazi wa ndani wa mbunge wa Jimbo la Moshi vijijini Cyril Chami
(CCM) aitwaye Mariam Said (16) amefariki dunia mapema alfajiri ya leo
ikiaminika kwabmba kifo chake kimesababishwa na kipigo toka kwa mke wa
Mbunge huyo.
Sababu kubwa ikielezwa kuwa binti huyo ambaye ni
muislamu alikataa kwenda kuhudhuria misa kanisani siku ya jumapili na
amekua na tabia ya kupinga kwenda kanisani kila mara tangu aajiriwe na
mbunge huyo kwa madai kuwa ni kinyume na imani yake (Uislamu).
Msimamo wa binti huyo ulimpelekea kipigo kikali usiku wa siku hiyo
(jumapili) ambapo inadaiwa alivunjika mbavu baada ya mke wa mbunge
kumpiga na stuli ubavuni.
Majirani wa mbunge huyo wanasema licha
ya binti huyo kuvunjika mbavu hakupewa matibabu yoyote badala yake
alifungiwa ndani huku akiendelea kulazimishwa kufanya kazi.
Mbaya
zaidi mke wa Mbunge huyo alimnyang'anya simu binti huyo ili asiweze
kuwasiliana na familia yake na kuwaeleza yaliyompata. Hata majirani
walipomuuliza juu ya hali ya mtoto huyo aliwajibu kwa lugha ya kejeli na
kuwaambia hakuna mtu anaweza kumfanya chochote, kwani serikali ni yao.
Kutokana na maumivu makali pamoja na kukosa matibabu hatimaye binti huyo
amefariki dunia leo asubuhi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment