Wema Sepetu a.k.a Beautiful Onyinye amekula kiapo cha kumchukia dada
wa hiyari wa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnum’, Halima
Kimwana ambaye wamekuwa na bifu kwa kipindi kirefu huku sababu zikiwa
hazijulikani.
Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Wema alisema ugomvi
wake na Halima Kimwana hautaisha na siku zote atamuonyesha chuki za wazi
sababu hana upendo naye hata kidogo.
“Kusema kweli yule dada namchukia mpaka basi, simpendi na sitompenda
kamwe, haitatokea hata siku moja kwenye maisha yangu nikapatana naye,
yaani suala la kupatana mimi na yeye halipo kabisa, hata yeye mwenyewe
anajua simpendi maana damu zetu zimekataana, siwezi hata kuonyesha
upendo wa maigizo kwake,” alisema Wema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment