UKATILI: MEYA AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MKEWE



Daniel Crespo enzi za uhai wake.
MEYA wa Bell Gardens, California nchini Marekani, Daniel Crespo ameuawa jana kwa kupigwa risasi na mkewe nyumbani kwake.
Crespo alipigwa risasi wakati wa mzozo baina yake na mkewe ambapo mtoto wao wa kiume mwenye miaka 19 alijaribu kuingilia na kusukumwa na baba yake ndipo mtuhumiwa alipofyatua risasi.
Marehemu alipoteza maisha akiwa njiani kupelekwa katika hospitali iliyo karibu na nyumbani kwake.
Mke wa marehemu,  Levette Crespo anashikiliwa na polisi kwa tukio hilo. 

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger