Muuza sura wa sinema za Kibongo, Wastara Juma amesema yupo kwenye
mikakati mizito ya kufanya mapinduzi kwenye tasnia ya filamu na
kutambulika kimataifa na ndiyo sababu ya kuanzisha Timu Wastara.
Akipiga stori na paparazi wetu, Wastara ambaye aliitendea haki sinema
ya Shaymaa, alisema soko la filamu Bongo bado lipo chini sana kwani
wasanii wengi wanajivunia kwa kujulikana majina bila manufaa ya kazi
zao, tofauti na nchi za nje ambao wasanii wake wanatambulika kwa kazi
zao.
“Wasanii wa Kibongo tuna umaarufu maandazi, tunajinadi kwa majina
siyo kazi ndiyo maana utakuta mtu ana umaarufu mkubwa lakini kazi zake
huzijui, madhumuni yangu ya kuanzisha hii timu ni kwa sababu nataka
kupambana niitoe nchi yetu kimasomaso na kukubalika kimataifa,” alisema
Wastara.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment