MADAMUUU! Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu
‘Madam’ amecharuka na kudai anachukizwa kwa kiasi kikubwa na wasanii
ambao wanapenda kumfanyia majungu kutokana na chuki zao binafsi.
Akipiga stori na paparazi wetu, Madam alisema anajua wapo wengi
wanaomchukia kutokana na sababu zisizo za msingi kwa kudai kuwa anaringa
na vyovyote vile wanavyojadili lakini hajali kwa kuwa hakuna ukweli
wowote.
“Watu wenye majungu hawanisumbui kichwa kabisa nabaki nawatazama tu,
sababu sina maringo wala majivuno kwa mtu yeyote, sasa cha ajabu wengine
wanasema naringa, kwa staili hiyo hatutafika mbali maana wasanii wa
nchi za wenzetu wana umoja hawana mambo ya aina hiyo,” alisema Wema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment