MAMA ALIYEVIMBA TUMBO AFARIKI DUNIA

YULE mwanamke aliyejulikana kwa jina la Mariam Manyata (57) ambaye aliandikwa kwenye gazeti hili  Toleo  Na. 838, Aprili 15  hadi  21, mwaka huu ukurasa wa 15 kwa kichwa cha habari HUU SI  UJAUZITO JAMANI, TUMBO  LIMEJAA MAJI, amefariki dunia.
Mariam Manyata enzi za uhai wake.
Mwanamke huyo (pichani) alifariki  dunia Mei 5, mwaka huu  katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jengo la Mwaisela  alipokuwa  akikendelea  na matibabu.
Lengo la habari  ile ya  kusikitisha lilikuwa  ni mwanamke huyo  kupata msaada baada  ya kukosa fedha kwa ajili ya matibabu akiwa katika hospitali hiyo.
Mariam alizikwa Mei 9, mwaka huu  kwenye Kijiji cha Mlodaa,  Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma  ambako ndiko alikokuwa akiishi.
Mwili wake kutoka Dar ulisafirishwa na Umoja wa Chama cha Iringa -Mvumi ambapo wakazi wake wanaishi Dar.
Gazeti hili linatoa  shukrani kwa Watanzania wote waliokuwa na nia ya  kumsadia Mariam lakini  Mungu amempenda zaidi.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger