CHUCHU ARINGISHIA PENZI LA RAY, ONA MWENYEWE HAPA

STAA wa filamu Bongo, Chuchu Hans amedhihirisha kwamba ana mahaba niue kwa mpenzi wake, Vincent Kigosi ‘Ray’ kwa kulinadi jina lake hadharani kwa kuvaa t-shirt iliyoandikwa; ‘Ray Kigosi’.
Staa wa filamu Bongo, Chuchu Hans akiringisha chata la msanii Mwenzake, 'Ray'.
Tukio hilo lilichukua nafasi wikiendi iliyopita kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini lililofanyika katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar ambapo mwanadada huyo aliambatana na mashosti zake kushuhudia burudani tofauti ikiwemo mechi ya timu ya Bongo Fleva na Movies anayoichezea mpenzi wake.
Chuchu Hans akipozi.
Chuchu alivaa t-shirt ya njano ambayo mgongoni ilikuwa imeandikwa Ray Kigosi kitu ambacho hakuwahi kukifanya kabla.“Sioni tatizo kujinadi hadharani, atakayemaindi shauri yake, nafanya kitu roho inapenda bwana sijali maneno ya watu hata kidogo,” alifunguka Chuchu.usiku wa matumaini 2014..

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger