JE, UNAMJUA DEMU MPYA WA DIAMOND PLUTNUM? NA UNAJUA KWAMBA WEMA ASHAURIWA KUJITOA MAPEMA ? HABARI KAMILI IPO HAPA

Yaliyomtokea  Miss  Tanzania  2006, Wema  Sepetu  mwaka  jana  huenda  yakajirudia mwaka  huu  baada  ya  kugundilika  mahusiano  mapya  baina  ya  Diamond   na  msanii  wa  muziki  aina  ya  Afro  Pop  na  mtangazaji  wa  kipindi  cha  Dance  100%  kinachorushwa  kupitia  kituo  cha  Televisheni  ya  vijana  EATV, Menina  Atick  a.k.a  Menina  la  Diva…..
Taarifa  toka  vyanzo  vya  kuaminika  zinadai  kuwa  Menina  hivi  sasa  ndo  binti  pekee  aliyeiteka  akili  ya  Diamond  kuliko  wote  waliowahi kuwa  naye  kimahusiano  huku  mama  mzazi  wa  Diamond  Bi, Snura  Kassim  akionekana  kumkubali  kwa  asilimia  zote  binti  huyo….
http://www.gumzolajiji.com/wp-content/uploads/2014/08/menina.jpg
Vyanzo  hivyo  vimebainisha  kuwa  mahusiano  ya  Menina  na  Diamond  yamekuwepo  kwa  miezi  kadhaa  sasa  na  Diamond  amekuwa  na  wivu  wa  kupindukia  juu  ya  demu  huyo  kuliko  inavyosemekana  kwani  amekuwa  akimfuatilia  kwa  kila  hatua….
“Hakuna  kitu  anachokifanya  Menina  kwa  sasa  Diamond  asijue, anampenda  vibaya  utadhani  karogwa  na  kuna  kipindi Diamond  alitaka  kumzuia  asijihusishe  na  chochote  kwenye  Dance 100%  kwa  kuhofia  kuporwa  lakini  baadae  alikubali  aendelee  na  Dansi  100%  baada  ya  kuhakikishiwa  na  dada  yake  Queen  Darling  ambaye  ni  mmoja  wa  majaji  katika  shindano hilo  kwamba atamlinda  asiguswe  na  mtu,” kimesema  chanzo  hicho.
Habari  zaidi  zinasema  kwamba  hata  hivi majuzi( kipindi  cha  mwezi  mtukufu  wa  Ramadhani)  Wema  alipigwa  marufuku  kushiriki  maandalizi  ya  futari  nyumbani  kwa  kina  Diamond  kwa  kigezo  kuwa  taratibu  za  dini  ya  kiislamu  haziruhusu  hawara  kumpikia  mwanaume  futari  lakini  Menina  alikuwa  akifanya  jambo  hilo  kwa  kujinafasi….
meninah
“Karibu  mwezi  mzima  Menina  alikuwa  akienda  kwa  kina  Diamond  na  kupika  futari, mbali  ya  hilo  alikuwa  akifanya  kila  alichokitaka  katika  nyumba  hiyo  pamoja  na  kufanya  usafi  katika  chumba  cha  Diamond,” kimesema  chanzo  chetu.

Hata  hivyo  chanzo  chetu  kimesema  kuwa  kuna  wakati  Diamond  aliwahi  kusikika  akisema  kuwa  hawezi  kumuoa  Wema  kutokana  na  rekodi  yake  ya  kuwahi  kuwa  na  mahusiano  na  watu  wengi  wanaojulikana  nchini  hivyo  kuwa  naye  kwa  ajili  ya  kujitangaza  kimuziki(  kumpatia  kiki)  tu  na  muda  wa  kuoa  utakapofika, ataoa  binti  asiye  na  umaarufu  jijini…..
Kibaya  zaidi  ni  kwamba  mama  Diamond  ameelezwa  kuwa  na  mapenzi  ya  dhati  na  Menina  jambo  ambalo  linamfanya  akose  raha  pindi  Wema  anapofika  nyumbani  kwake…
Diamond  alipotafutwa  kupitia  simu  yake  ya  mkononi  ili  kuzungumzia  jambo  hilo, simu  yake  iliita  bila  kupokelewa. Wema  hakupatikana  katika  simu  zake  zote.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger