MWENYEKITI WA BUNGE LA KATIBA AUNDA TUME YA WATU 6 ITAKAYOTAZAMA JINSI YA KUONGEZA POSHO SH. 300,000 KWA SIKU


Suala la posho limezidi kuwa kaa la moto katika vikao vya Bunge la Katiba vinavyoendelea mjini Dodoma leo, hali iliyomlazimu mwenyekiti wa muda, Pandu Ameir Kificho ateue timu maalum ya watu 6 kutazama jinsi ya kuboresha viwango vya posho hizo. 
 
Timu hiyo inatarajiwa kuyachunguza kwa undani mahitaji ya wajumbe wa Katiba, kisha kuisaidia serikali kutafuta jinsi ya kuongeza posho hizo.
 
Wajumbe wa timu ya posho ni pamoja na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.
 
Wengine ni mjumbe wa asasi zisizo za kiserikali Paul Kimiti, Mbunge wa Peramiho Jenister Mhagama (CCM) na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Asha Bakari na Mohamed Aboud Mohamed.
 
Huku hayo yakiendelea Dodoma, Katibu Mkuu wa Chadema Dr Wilbrod Slaa amedai  kuwa posho wanayopewa wajumbe ya Sh 300,000 kwa siku inatosha kabisa, “kwa kuwa hata wafanyakazi wengine wa serikali wanapokea mshahara wa laki tatu mwisho wa mwezi.”
 
Mwenyekiti Msaidizi wa CUF, Julius Mtatiro anaunga mkono mtazamo huu. Katika waraka wa wazi aliouweka kwenye ukurasa wake wa Facebook, Mtatiro anaandika:
 
“Shilingi laki tatu tunazopewa kwa siku zinatosha kabisa, ambaye hazimtoshi aongeze za kwake [ama] aondoke Dodoma ili kupisha wanaoweza kutunga katiba kwa posho ya Sh 300,000 waendelee.”

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger