JB APEWA MAKAVU LIVE NA MTITU


Stori: Mwandishi Wetu
KATIKA hali ya kushangaza msanii wa filamu na Mkurugenzi wa Five Effect, William Mtitu amemchana live msanii mwenzake, Jacob Stephen ‘JB’ baada ya kutoa mchango mdogo kwenye msiba wa Sheila Haule ‘Recho’.
Msanii wa filamu na Mkurugenzi wa Five Effect, William Mtitu (wa tatu kutoka kushoto) akiwa karibu na jeneza la Recho Haule.
Akizungumza msanii mmoja wa filamu ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, alisema katika kutoa michango ya msiba wa Recho ilifika zamu ya JB ambapo alichangia elfu hamsini jambo ambalo lilimkera Mtitu na kuanza kumchana live.
JB na Mtitu wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, paparazi wetu alimuuliza Mtitu kulikoni ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Ukweli iliniuma sana ndiyo maana nikaamua kumchana JB mbele za wasanii yaani msanii mkubwa kama yeye na analipwa vizuri lakini anakuja kutoa shilingi elfu hamsini hii siyo sawa japo alikasirika lakini ujumbe ulifika

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger