LUCY KOMBA: NIACHENI NIMCHUNE MZUNGU

MSANII
wa filamu za Kibongo, Lucy Komba amefunguka aachwe adendeke hadharani na mpenzi wake Mzungu Janus kwani ni mtu mwenye malengo naye.
Msanii wa filamu za Kibongo, Lucy Komba akiwa na mchumba wake aliyetambulika kwa jina la Janus.
Akizungumza na mwandishi wetu mara baada ya kuhojiwa juu ya picha zilizozagaa mitandaoni, Lucy alisema kuwa picha hizo alizipiga akiwa na mchumba wake huyo kwa hiari yake.
“Huyo mzungu ni mchumba wangu wa siku nyingi anaitwa Janus, tunapendana sana ndiyo maana sijaficha kitu niliamua kuziweka picha hizo kwenye ukurasa wangu wa Instagram. Niacheni nifanye yangu,” alisema Lucy.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger