MIKE AIPOTEZEA TAFF, AJIUNGA BONGO MOVIE

MUIGIZAJI
wa sinema za Kibongo, Michael Sangu ‘Mike’ amejiuzulu ujumbe wa Bodi ya Shirikisho la Filamu (TAFF) na kujiunga rasmi na Klabu ya Bongo Movie.
Muigizaji wa sinema za Kibongo, Michael Sangu ‘Mike’.
Akizungumza na paparazi wetu, Mike alisema amefikiri kwa kina na kuona bora ajiengue katika Taff na badala yake aelekeze nguvu zake katika Klabu ya Bongo Movie ambayo anaamini kwa sasa ni sahihi kwake.
“Nimeamua mwenyewe, sijalazimishwa na mtu, kila mtu na maamuzi yake, acha kwa sasa niwe Bongo Movie kwani kila kitu kinakwenda na wakati,” alisema Mike.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger