MSICHANA ALIYEPIGWA NA CHID ATIMKIA SAUZI

MSICHANA aliyewahi kupigwa na msanii wa Hip Hop Bongo, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’, Mwanaisha Sued ‘Aisha’ ametimkia nchini Afrika Kusini kuishi kwa muda.
Mkali wa Hip Hop Bongo, Rashid Makwiro ‘Chid Benz’,
Paparazi wetu alitia timu nyumbani kwa binti huyo Ilala-Bungoni, jijini Dar ili kujua maendeleo yake ambapo mdogo wa Asha ambaye hakutaka jina lake lichorwe gazetini, alijibu kwa kifupi:
“Aisha hayupo amekwenda Sauzi kwa muda, kuhusu alichokifuata mimi sijui. Ila hajambo na anaendelea vizuri.”

Aprili mwaka huu, Chid Benz alishtakiwa katika kituo cha Polisi cha Pangani, Ilala kwa kosa la kumshambulia Aisha ambaye aliwahi kuwa mpenzi wake.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger