MUME AMCHARANGA MAPANGA NA KUMPIGA MAPANGA MKEWE HUKU AKIWA NA MIMBA YA MIEZI 6, KISA WIVU WA MAPENZI

Ni jambo la kawaida kuwaona wanaume  wilayani Serengeti wakiongozana na wake ama watoto wao siku za minada,  kwenda kuuza mifugo ili wanunue mahitaji yao, lakini mapato hudhibitiwa na wanaume.
Mara baada ya mauzo na kununua mahitaji,wanawake na watoto hulazimika kurudi nyumbani huku wanaume wakibaki wakistarehe ,huzitumia siku ,ni nadra mwanaume kuwahi kurudi nyumbani .
Mei 19, Rhoda Nyangi Mtatiro (24) mkazi wa Kitongoji cha Kenyana kijiji cha Masangura kata ya Ring’wani wilayani Serengeti, licha ya ujauzito  wa miezi sita alionao alikubali kuongozana na mumewe Wang’enyi Sabai(30) kutoka kijijini kwao hadi Rung’abure umbali wa kilometa zaidi ya 15 kwa mguu.
Huku wakiswaga kondoo wanne walifanikiwa kufika mnadani na kuwauza  wakajipatia  fedha za mahitaji hakujua kuwa  kuna balaa lingemkuta  siku hiyo, pamoja na kuswaga na kutembea umbali mrefu na ujauzito wake hakuambulia kitu zaidi ya kipigo ambacho leo hajui hatima ya maisha yake.
Rhoda akionyesha majeraha kwenye sehemu ya mwili wake yaliyotokana na kipigo cha mumewe
Rhoda akionyesha majeraha kwenye sehemu ya mwili wake yaliyotokana na kipigo cha mumewe
Licha ya kufanikiwa kuuza kondoo wote aliambulia  Sh 2,000 kwa ajili ya kununua nguo za mtoto wao mmoja kati ya wanne walionao anayesoma darasa la kwanza shule ya Msingi Geitasamo, iliyoko hapo Rung’abure ambako ni kwao na Rhoda.Ilikuwaje?
“Nilizunguka kutafuta nguo za mtoto, wakati huo mume wangu alikuwa nyumbani kwetu anamsalimia mama mkwe…. Saa 11:30 jioni nilifika nyumbani na kuwaambiwa ameishaondoka kurudi kijijini kwetu….nilishindwa kuondoka pekee yangu kwa muda huo na hali niliyonayo nikalala kwetu, ikawa mwanzo wa matatizo,”anasema.
Anasema alilazimika kutoka saa 12 alfajiri na kufika kwake saa tano asubuhi akiwa amechoka ,na kwenda kumsalimia mume wake dukani, hata hivyo alivyopokewa akahisi atapata adhabu kwa kuwa mume wake hana namna nyingine ya kuwasilisha hisia zake zaidi ya kutembeza kipigo, akaamua kuaga na kurejea nyumbani.
“Nilishangaa kuona mume wangu akifunga duka huku akiwa ameshikilia panga na kamba ananifuata …mita kadhaa akanifikia na kuniamru nisimame, eneo lenyewe limejaa vichaka….niliingiwa na hofu, ghafla akauliza nilikolala…kwa kujiamini nikamwambia nililala nyumbani kwetu baada ya kuogopa kutembea pekee yangu jioni,” anasema na kuongeza:
“Akasema ameambiwa nilikuwa na mwanaume gesti….nilimtaka anielewe kuwa nililala kwetu baada ya kuniacha…na ujauzito huo ninawezaje kwenda na mwanaume gesti….ikawa kama amechokozwa maana aliniamuru ninyanyue mikono juu na kuanza kunishambulia kwa mateke tumboni, kama vile haitoshi akaanza kunikata miguu kwa panga ili niseme kuwa nilikuwa na mwanaume gesti,” anasema kwa masikitiko.

Afungwa kwenye kiti

Pamoja na maumivu ya kupigwa tumboni na kukatwa miguu, alifungwa kwenye kiti na kuendelea kuadhibiwa mbele ya mama mkwe wake Rhobi Sabai na mke Mwenzake Rhobi Kibina(20), hadi akapoteza fahamu, hata hivyo alijikuta amefungiwa ndani ya nyumba na kuambiwa kuwa aliokolewa na jilani yao Moya Marwa.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger