ESHA BUHETI AAPA KIAPO CHA KIFO, SOMA ZAIDI HAPA

MUIGIZAJI Bora wa Kike 2014 kupitia Tuzo za Zanzibar Film Festival (Ziff), Esha Buheti ameapa kuwa iwapo atakuja kujichora tatuu au kufanya mapenzi ya jinsia moja, Mungu aingamize familia yake na kizazi chake chote.
Muigizaji Bora wa Kike 2014 kupitia Tuzo za Zanzibar Film Festival (Ziff), Esha Buheti
Esha alitoa kiapo hicho juzikati alipokuwa akijibu swali aliloulizwa na paparazi wetu kuhusiana na tuhuma za kudaiwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja zilizotua kwenye dawati la Risasi Jumamosi.
“Mimi ni mtoto wa Kiislamu na nina maadili yote ya dini, siwezi kujihusisha na mapenzi ya kinyume cha maumbile, mapenzi ya jinsia moja,” alisema.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger