Nicola
Rizzoli amechaguliwa na Fifa kuwa mwamuzi katika mchezo wa fainali -
Kombe la Dunia Brazil 2014 kati ya Ujerumani na Argentina.
Howard Webb kutoka England, aliyechezesha fainali ya Kombe la Dunia 2010 Afrika Kusini, aliorodheshwa lakini hakuchaguliwa.
Ujerumani itapambana na Argentina kwenye dimba la Maracanã, jijini Rio De Janeiro, siku ya Jumapili Julai 13.
Rizzoli ni msanifu majengo kutoka Bologna, na tayari amechezesha mechi tatu katika michuano ya Kombe la Dunia Brazil.
Mwamuzi huyo mwenye umri wa miaka 42
alichezesha mechi kati ya Spain dhidi ya Uholanzi, Nigeria na Argentina
na Argentina ilipocheza na Ubelgiji.
Rizzoli pia alichezesha mchezo wa
fainali ya Ligi ya Europa kati ya Atlètico Madrid dhidi ya Fulham mwaka
2010, na pia mchezo wa fainali ya Uefa Klabu Bingwa Ulaya mwaka 2013
kati ya Bayern Munich na Borussia Dortmund.
Rizzoli atasaidiwa na waamuzi wa
pembeni Renato Faverani na Andrea Stefani, na mwamuzi wa nne atakuwa
Carlos Vera kutoka Ecuador.
Rizzoli atakuwa mwamuzi wa tatu
kutoka Italy kuchezesha fainali, baada ya Sergio Ginella mwaka 1978 na
Pierluigi Collina mwaka 2002.
No comments:
Post a Comment