IFAHAMU HISTORIA YA REFA ATAKAYE CHEZESHA FAINALI ZA FIFA 2014, ANATOKA ITALY

Nicola Rizzoli amechaguliwa na Fifa kuwa mwamuzi katika mchezo wa fainali - Kombe la Dunia Brazil 2014 kati ya Ujerumani na Argentina. 

Howard Webb kutoka England, aliyechezesha fainali ya Kombe la Dunia 2010 Afrika Kusini, aliorodheshwa lakini hakuchaguliwa. 

Ujerumani itapambana na Argentina kwenye dimba la Maracanã, jijini Rio De Janeiro, siku ya Jumapili Julai 13. 
Rizzoli ni msanifu majengo kutoka Bologna, na tayari amechezesha mechi tatu katika michuano ya Kombe la Dunia Brazil.

Mwamuzi huyo mwenye umri wa miaka 42 alichezesha mechi kati ya Spain dhidi ya Uholanzi, Nigeria na Argentina na Argentina ilipocheza na Ubelgiji. 

Rizzoli pia alichezesha mchezo wa fainali ya Ligi ya Europa kati ya Atlètico Madrid dhidi ya Fulham mwaka 2010, na pia mchezo wa fainali ya Uefa Klabu Bingwa Ulaya mwaka 2013 kati ya Bayern Munich na Borussia Dortmund.
 
Rizzoli atasaidiwa na waamuzi wa pembeni Renato Faverani na Andrea Stefani, na mwamuzi wa nne atakuwa Carlos Vera kutoka Ecuador. 

Rizzoli atakuwa mwamuzi wa tatu kutoka Italy kuchezesha fainali, baada ya Sergio Ginella mwaka 1978 na Pierluigi Collina mwaka 2002.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger