UTAPELI
sasa wachukua sura mpya mkoani Iringa bada ya baadhi ya waganga wa
tiba asilia (Sangoma) kugeuziana kibao wenyewe kwa wenyewe kwa
kuanza kufanyiana utapeli wa kutisha ikiwa ni pamoja na kujifanya
maofisa wa polisi na kuwatapeli fedha wenzao zaidi ya 60.
Imedaiwa
kuwa waganga hao matapeli wana mtandao wao na wamekuwa wakiwatumia
askari wasio na maadili ya jeshi la polisi kwa kwenda kuwatisha
waganga wachanga kwa madai kuwa wao ni maofisa wa polisi na serikali
ambao wanafuatilia leseni zao za kazi na kuwatisha kuwa wanafanya
kazi kienyeji hivyo wanapaswa kufikishwa polisi na wakiwa njiani
wanawataka kutoa rushwa kati ya 300,000 hadi milioni moja ama kuingia
nao makubaliano ya mkopo ya fedha hizo za rushwa kabla ya kuwaachia.
Katibu
wa chama cha wanganga wa tiba asilia wilaya ya Iringa Dr Salum
Kalolo (pichani) alithibitisha jana kuwepo kwa utapeli huo na
kuwatayari chama chake kimeanza kuchukua hatua ya kuwasaka matapeli
hao ambao tayari baadhi yao majina yao yanafahamika na wanaendelea
kusakwa ili kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Dr
Kalolo alisema kuwa awali utapeli huo ulikuwa ukifanyika chini
kwa chini na ili kuwa ni siri ila kwa sasa utapeli huo umeendelea
kufanyika wazi wazi na tayari kama chama kimeona ni tatizo kubwa
ina iwapo watanyamaza kimya madhara yanaweza kuwa makubwa zaidi .
"
Tunasikitika sana kuona kuwa waganga wa tiba asilia wameacha
kufanya kazi yao ya uganga na wamejiingiza katika wimbi la utapeli
wa kuwatapeli wanganga wenzao fedha kwa kutumia njia ya vitisho mbali
mbali.....tena mbaya zaidi wanawatumia baadhi ya askari kufanya
utapeli huo"
Alisema
kuwa waganga hao matapeli wamekuwa wakijipachika vyeo mbali mbali
zikiwemo vya polisi na maofisa wa serikali kupitia wizara ya afya
kwa madai wametoka makao makuu na wapo mkoani hapa kwa ajili ya
kufanya ukaguzi mbali mbali kwa waganga wa tiba asilia jambo ambalo
si kweli bali wamelenga kujipatia fedha kwa njhia ya udanganyifu
Dr
Kalolo alisema kuwa tayari waganga zaidi ya 60 wametapeliwa
katika Manispaa ya Iringa , Kilolo ,Iringa vijijini na wilaya ya
Mufindi na kuwa wao kama chama wamekwisha wakamata baadhi ya
wanganga hao na pindi wanapowafikisha polisi wamekuwa wakiachiwa
huru .
Hivyo
ameliomba jeshi la polisi na serikali ya wilaya na mkoa kusaidia
kukomesha utapeli huo ili kuepusha madhara zaidi kujitokeza mkoani
Iringa.
Mbali
ya kuomba jeshi la polisi na serikali kusaidia kukomesha tabia hiyo
pia alisema hatua ambayo chama chake kimechukua ni pamoja na
kuendesha zoezi la kuyaondoa barabarani na mitaani mabango yote
ambayo yamewekwa na waganga hao wasio fahamika .
Wakati
huo huo chama hicho cha wanganga wa tiba asilia wilaya ya
Iringa kimeiomba serikali kuangalia uwezekano wa kutenga bajeti
kifedha kwa ajili ya wanganga hao kupitia vyama vyao ili
kuendelea kuboresha zaidi huduma yao .
.
Kwani
alisema huduma ambazo wanganga hao wanazitoa ni kwawananchi wa
Tanzania hivyo kama ilivyo katika sekta ya afya ambazo zimekuwa
zimekuwa zikitengewa bajeti.
No comments:
Post a Comment