MSANII mkongwe wa filamu Bongo, Sabrina Rupia
‘Cathy’ amefunguka kuwa anakerwa na tabia za mawifi kuwachukia wake za
kaka zao bila sababu za msingi.
Akichonga na paparazi wetu, Cathy alisema mawifi wengi huwachukia na
kuwawekea vinyongo wake wa kaka zao hata kama hawajawakosea, kitu
ambacho kinamkera na anaamini siyo yeye peke yake, bali jamii nzima
inachukia tabia hizo.
“Ukweli nakerwa sana, yaani utakuta wanakuchukia bila sababu, muda
mwingine wanakuwa na vinyongo mioyoni na kusema maneno yasiyofaa ya
kukuponda, hawajui kwamba nao ni binadamu kama walivyo wao, naomba
waache tabia hii, siyo nzuri,”alisema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment