Showing posts with label CATHY. Show all posts
Showing posts with label CATHY. Show all posts

CATHY:JAMANI BONGO MUVI INAKUFA

MSANII wa filamu ambaye pia ni mweka hazina msaidizi wa klabu ya Bongo Movie Unity, Sabrina Rupia ‘Cathy’ amefunguka kwamba anaona kundi hilo linakwenda kufa na halitakuwepo kabisa kutokana na kujiuzulu kwa mwenyekiti wao, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Msanii wa filamu Bongo Movie Unity, Sabrina Rupia ‘Cathy’.
Akistorisha na paparazi wetu, Cathy alisema amejisikia vibaya Steve Nyerere kujiuzulu na wao kama viongozi hawakuwa na taarifa hivyo kutokana na kwamba kiongozi huyo alikuwa mpiganaji Bongo Movie itakufa kwani hakuna mtu anayeweza kuongoza kama Steve.
“Steve yeye kama binadamu ana mapungufu kidogo lakini mazuri aliyofanya ni mengi kwani alikuwa mpenda maendeleo lakini kujiuzulu kwake ni pigo na ninaona kama kundi hili halitakuwepo tena, yaani ninajisikia vibaya sana na amejiuzulu ghafla mno,” alisema Cathy.
Read more >>

MAWIFI WAMKERA SANA CATHY

MSANII mkongwe wa filamu Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ amefunguka kuwa anakerwa na tabia za mawifi kuwachukia wake za kaka zao bila sababu za msingi.
Msanii mkongwe wa filamu Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’
Akichonga na paparazi wetu, Cathy alisema mawifi wengi huwachukia na kuwawekea vinyongo wake wa kaka zao hata kama hawajawakosea, kitu ambacho kinamkera na anaamini siyo yeye peke yake, bali jamii nzima inachukia tabia hizo.
“Ukweli nakerwa sana, yaani utakuta wanakuchukia bila sababu, muda mwingine wanakuwa na vinyongo mioyoni na kusema maneno yasiyofaa ya kukuponda, hawajui kwamba nao ni binadamu kama walivyo wao, naomba waache tabia hii, siyo nzuri,”alisema.
Read more >>

CATHY ASEMA: AKIWA STAA HALAFU UKIWA UMEOLEWA BASI NI MAJANGA TU



MSANII maarufu katika tasnia ya filamu Bongo, Sabrina Rupia ’Cathy’ amewataka wasanii wenzake kutofanya ustaa kwenye ndoa zao kwani ndiyo chanzo cha kuvunjika kwa ndoa nyingi.
Msanii maarufu katika tasnia ya filamu Bongo, Sabrina Rupia ’Cathy’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Cathy alisema kabla ya kuolewa lazima uwe na utayari wa kuolewa na kujuana kwa undani zaidi na mwenzio kabla ya kufanya uamuzi pia usiweke neno kuachika katika ndoa kwa sababu tu unaweza kupata mwingine.
“Uvumilivu ndiyo nguzo muhimu katika ndoa, unapojifanya staa na kuishi maisha ya kistaa katika ndoa, mambo yanaharibika kabisa,” alisema Cathy huku akikataa kutoa mifano ya walioachika kwa kuendekeza ustaa katika ndoa akidai wanajijua.
Read more >>

CATHY AFUNGUKA SABABU ZA KUPENDA KUZIDIWA UMRI NA MUMEWE

TUNAMALIZIA makala haya ya Sabrina Rupia ‘Cathy’ tuliyoyaanza wiki tatu zilizopita, mwigizaji huyu alifunguka mambo mengi kuhusiana na maisha yake, bila shaka kupitia mfululizo wa makala haya, msomaji utakuwa umejifunza vitu vingi kutokana na hatua ambazo amepitia maishani na leo hapa anafunguka kuhusu  anavyofurahia maisha ya ndoa kwa kuolewa na mume ambaye amemzidi umri SHUKA NAYO…
Msanii mkongwe katika fani ya maigizo Bongo, Sabrina Rupia ‘Cathy’
Mwandishi: Kwa nini ulipenda mumeo akuzidi umri?
Cathy: Kwanza nilipenda busara zake na namna anavyonilea kama mtu wake wa karibu, si mtu wa mbwembwe kama walivyo wengine, namfurahia kwa sababu tunafanya maisha ya kweli, lakini nilitaka kupata mwanaume mwenye huruma ambaye hatoniumiza kama wafanyavyo vijana kwa sababu ya maisha ambayo nimeyapitia ya kuwa mpweke baada ya kufiwa na baba yangu.

Mwandishi: Una watoto wangapi kwa sasa?
Cathy: Sipendi kutaja watoto ila fahamu ni mama wa familia.
Mwandishi: Je ndoa uliyonayo ni ya ngapi kwako?
Cathy: (Anatahamaki kidogo) We! Ndoa ya ngapi? Hii niliyonayo ni ya kwanza na mwisho!
Mwandishi: Vipi kuhusu mameneja wako katika kazi za uigizaji hawakusumbui suala la kukusimamia bila kuwapa tunda la mumeo.

Cathy: Hapana najitambua lakini pia najivunia kuwa mme wangu ndiye meneja wangu kwa hiyo tunda ni halali yale kabisa.
Mwandishi: Ni kweli Bongo Muvi hamko tayari kuwatoa wasanii wachanga?
Cathy: Kwa kifupi hela zinaenda kwa wenye hela, hata mimi naweza kulalamika lakini nikipata nitachukua waliopata wenzangu na kuwaongezea na wale wapambane kutoka.
Mwandishi: Kwa nini msibebane?

Cathy: Ninachojua cha msingi ni kufaiti unavyojua mwenyewe lakini usikae kwa kumsubiri flani atoke ili akupe kiki hakuna mtu wa kukufanyia hivyo.
Mwandishi: Duuh! Kwa hiyo kila msanii anatakiwa kujibeba kivyake?
Cathy: Nafasi huwezi kupewa cha msingi ni kupigana na kutafuta upenyo wa kutoka iwe kwenye muvi au nje ya sanaa.

Mwandishi: Mpaka sasa una filamu ngapi?
Cathy: Kama nne au tano, kuna DNA, Wheel Chair nilifanya na Cloud, Saa Nne, Kaburi na Simu ya Mkononi ambazo hazijatoka.
Mwandishi: Nini ushauri wako?

Cathy: Watu wasibweteka hasa kina dada watumie nguvu zao kufanya kazi lakini pia wasanii wachanga wafaiti wenyewe wasisubiri kuolewa, kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake.
Mwandishi: Unazungumzije suala la ajira kwa vijana?

Cathy: Wanyanyuke waache uzembe kwani hata kilema anatamani japo anyanyuke kwa dakika kadhaa ili atembee, asiye na mikono anatamani angekua nayo ili imsaidie japo kulima sembuse wewe uliyekamilika unashindwa kujisaidia mpaka usubiri kutolewa!
             Mwisho.
Read more >>
 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger