MTOTO MWENYE UGONJWA HUU APATA MATUMAINI

Habari hiyo ilimhusu mtoto Salum Kassim wa miaka 16 anayesumbuliwa na tatizo la tumbo kujaa maji na kulifanya kuwa kubwa sana huku madaktari wakisema chanzo ni hitilafu kwenye moyo.
Salum Kassim anayesumbuliwa na tatizo la tumbo kujaa maji.
Baada ya maelezo ya mtoto huyo kuhusu ugonjwa huo mbaya na maisha duni anayoishi, ilionekana kuwa mlezi wake amekuwa akitumia shilingi elfu kumi (10, 000) kila mwezi kununua dawa za kutuliza maumivu anayoyapata na si kumaliza tatizo.
Hata hivyo, kuna mwezi mtoto huyo anapitiliza bila kupata dawa baada ya mlezi wake kutokuwa na kiasi hicho cha pesa hali inayomsababishia kupoteza mpangilio wa dozi.
Mwisho wa habari tuliandika namba za simu za mlezi wa mtoto huyo kwenda kwa Watanzania watakaoguswa na afya tete ya Salum kumchangia ili aweze kupata tiba sahihi na hivyo kuokoa uhai wake ambao upo hatarini kwa mujibu wa madaktari.

Mtoto Salum Kassim akiwa nyumbani kwao
Sasa kwa mujibu wa mlezi wa mtoto huyo, tangu gazeti hilo kutoka mpaka juzi, Julai 8, mwaka huu wasamaria wema wamejitokeza kumsaidia mtoto huyo ambapo kiasi cha shilingi 300,000 zimeshachangwa huku wengine wakiahidi. Hii ni dalili njema!
Aidha, Julai 2, mwaka huu, waandishi wa Global walikwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili Kitengo cha Magonjwa ya Moyo kwa lengo la kuangalia uwezekano wa kumpeleka mtoto Salum kuanza vipimo lakini daktari mmoja alisema atatoa jibu lini apelekwe bila kufafanua sababu za kusema hivyo licha ya Rais Jakaya Kikwete wakati wa ufunguzi wa taasisi hiyo kutoa maelekezo kwamba, iwasaidie Watanzania, hasa walalahoi, bila kuweka vikwazo.
Muonekano wa tumbo la Salum Kassim
Mlezi wa mtoto huyo amesema kuwa, licha ya maradhi yanayomsumbua Salum, anakabiliwa na changamoto zingine zinazohitaji kutatuliwa kwa fedha kama chakula, sabuni, mafuta ya kupaka mwilini, maji ya kunywa, dawa ya meno pamoja na mavazi.
Ili kumsaidia mtoto Salum, endelea na moyo wa kutoa kwa kutuma kiasi chochote cha pesa kwenda namba 0785 999 276 na 0682 865248. Namba zote ni za mlezi wa mtoto huyo. Magazeti ya Global yataendelea kutoa maendeleo yake kila wakati.
Ndugu msomaji, kumbuka kutoa ni moyo hivyo msaidie mtoto huyu upate baraka. Mhariri.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger