TUTAENDA KUTUMBUA BAADA YA KUUZA VITUMBUA


Oya masela vipi? Ama nini wazazi? Inakuwaje makachaa wangu? Kama kawa kama dawa kitaa hii ni supa kabisa yaani kutoka kwenye maganda yake. Ama nini? Kitaa hiyo barida? Kaa hapo upate hizi tamu arifu.
Tudei bana ngoja nikisanue na sadi stori ya mtu wangu wa nguvu Luka. Jamaa alipokuwa na eji ya miaka bee tu, maza’ke alidedi aisee.
Bimkubwa alikuwa amezinguliwa na kansa foo meni yiazi na mwishowe alidanja. Lilikuwa pigo hatare kwa mwanangu Luka kozi alikuwa hajafikia eji ya kulimudu hili laifu. Si unajua zile za kuachwa yatima ukiwa janki?

Baada ya parenti huyo mmoko kutangulia mbele ya haki, aisee jamaa anakuteli kuwa haukupita mwaka mmoko, dingi naye akakata ringi mazee. Mshua alipata ugonjwa ulioafekti figo dheni akatangulia. Sasa ndiyo selaa wangu Luka akagundua kuwa amebaki aloni. Dah! Kachaa unaambiwa pamoko na eji ndogo bati alitamani ardhi ipasuke azame insaidi asiione shruba iliyokuwa mbele yake.
Chuma anarimemba kuwa sista’ke alikuwa ndiyo kwanza anamaliza standadi seveni. Anakuteli kwamba ndugu wa mdingi ambao ni masnichi waliwanyang’anya mali zote yakiwemo mashamba, viwanja, mifugo hata mahausi ambayo maparenti waliyaacha.
Skuli walipigwa chini fasta na kupelekwa kileji kuchunga mifugo kwa magrendi parenti. Hivyo ndivyo drimu za mwanangu Luka zilipotaka kuyeyuka bati mwana hakukata tamaa, ndiyo kwanza aliendelea kuwaza kuwa pamoja na kukosa shule ipo dei atakuwa bonge la mtu kwenye sosayati.
Jamaa anakuteli kuwa hakuna kichwa kilichowajali so wakajikuta wakijiokotea tu kama makinda wa ndege waliotelekezwa na mama zao. Mnanisoma wanangu? Nanyaka kuwa unajiuliza kuwa msela anataka kusema nini? Tulia upate pointi.

Kwa kuwa mtu wangu wa nguvu Luka ndo alikuwa janki pale skani kileji basi jobu aliyopangiwa ilikuwa ni kuchota wote kupiga usafi na ikawa ratiba yake ya deile.
Mwana anafunguka kuwa hakuna ndugu aliyejua wamepiga menyu au kudeshi. Unajua shida wewe? Kama umezaliwa maghorofani na kupanda mboga kwenye makopo huwezi kung’amua ninachokizungumzia. Kaa hapo wewe.

Unajua katika kusovu laifu gumu pale skani ilibidi sista yao akafaindi jobu za ndani akawa anapiga mbishe za uhausigeli.
Selaa anaamplifai kuwa maparenti zake walikuwa na washkaji zao kibao bati baada ya wao kudanja, mwanzoni walimlipia sista yao ada ya skonga. Bati taimu ilipozidi kusonga ndivyo walivyokuwa wakiyeyuka mmoko baada ya mwingine.
Kuna taimu jamaa yangu aliumwa kinoma bati wale relativu wa mshua wake hawakujali. Kuna mmoko alimteli kuwa kama vipi naye adanje kama ilivyokuwa kwa maparenti zake kwani alidizevu tu!
Baada ya kuona dhiki na njaa kama Somalia huku akiwa amedhoofu afya hatare. Mwanangu alikuwa akigonga vibarua vya kulima ili angalau mkono uende kwa kinywa.

Samtaimu alikuwa akizinguliwa na malandi lodi. Si unajua zile za kwanza hujalima freshi ooo rudia fulu mizinguo daadeki! Kachaa aliitwa kila taipu ya jina baya pale kitaa kisa tu poveti, aisee usiombe ukawa maskini kozi ni adhabu tosha hapa duniani.
Sikia stori hii, unaambiwa ukimtendea mtu ubaya malipo ni hapahapa anda dhe sani. Haikuchukua taimu ndefu baadhi ya wale ndugu masnichi waliokuwa wakiwanyanyasa mshikaji na ndugu zake zake aisee unaambiwa walianza kupukutika au kudanja mmokommoko.
Ndichi wangu hakukata tamaa kozi alitafuta kitu cha nauli na kuzama tauni kisha akaanza kuhaso. Tudei ametusua, baadhi ya ndugu wa mshua waliobaki, ndiyo wanabisha hodi deile kuomba msosi wakiwa wamejawa na nishai usoni. Mmenisoma wazazi? Acha tuuze vitumbua dheni ndo tukatumbue! Haso zetu ndizo zimetufikisha hapa tulipo.
Sii yuu neksti wiki. Mia!

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger