STAA wa filamu Bongo, Baby Joseph Madaha amemwagana
na aliyekuwa mwandani wake ambaye pia ni meneja wake, Joe Kairuki
pasipokuwa na sababu za wazi.
Chanzo chetu cha kuaminika kilichoomba hifadhi ya jina lake
kimetutonya kuwa, Madaha na Joe wamebaki kuwa mtu na bosi wake ila
msanii huyo sasa amejiweka kwa mwanaume mwingine.
Katika kujua ukweli wa ishu hiyo, mwandishi wetu alimpigia simu
Madaha ambaye alisema: “Hee unaniuliza kuhusu Joe, mbona umechelewa
kujua? Nimeachana naye, sasa nimejipatia mpenzi wangu mwingine na
tunapendana kupita maelezo.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment