UKATILI: MWANAMKE ATEKWA, AUAWA, MAITI YALIWA NA MBWA

MAMA mmoja mkazi wa Kijiji cha Bago, Kata ya Kiwangwa Tarafa ya Msata wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani aliyefahamika kwa jina la Asha Mrisho (pichani), amekutwa ameuawa na kufukiwa kwenye shamba la mananasi.
Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Bago, Maulid Omary Tamla akionesha sehemu alipofukiwa marehemu Asha Mrisho kwa mara ya kwanza .
Katika tukio hilo, mama huyo inadaiwa  aliaga kuwa anakwenda Mbande, Dar es Salaam kwenye harusi ya ndugu yake ambayo ilifanyika Juni mwaka huu.Wifi wa Asha, Cheka Mrisho aliliambia gazeti hili kuwa marehemu aliondoka nyumbani na hakuna aliyekuwa na wasiwasi kwa vile walielewa alikuwa harusini.
Aliongeza kuwa, baada ya kuona kimya, mtoto wake alipiga simu kwa ndugu zake wanaoishi Dar na kuulizia alipokuwa mama yake, alifahamishwa kwamba  hakuonekana ndipo jitihada za kumtafuta zikaanza bila mafanikio.

Marehemu Asha Mrisho enzi za uhai wake.
Cheka alisema: “Kabla ya kuondoka Juni 26, mwaka huu, Asha alifanya mawasiliano na mtu ambaye simjui, hivyo nina wasiwasi huenda alitekwa.”Asha alipatikana Julai 28, mwaka huu baada ya siku 32 kupita akiwa amefariki dunia na kufukiwa katika shamba la mananasi la mtu aliyetajwa kwa jina la Abdallah Muligazi.
Hii ni nyumba aliyokuwa anaishi marehemu.
“Marehemu aligundulika na mbwa ambao walikuwa wakimnyofoa viungo vya mwili wake huku wakibweka na mfanyakazi wa shamba hilo aitwae Rashidi Ally alipokwenda kuangalia kuna nini, akaikuta maiti ikiwa imefukuliwa,” alisema Asha.
Wifi wa Asha, Cheka Mrisho.
Ally alitoa taarifa kwa uongozi wa kijiji ambao uliita polisi na mwili ulipofukuliwa ulitambuliwa kuwa ni wa Asha, baada ya uchunguzi wa madaktari, wakaruhusu azikwe.Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Bago, Maulid Omary Tamla aliliambia gazeti hili kuwa habari za marehemu kupotea zilifikishwa ofisini kwake siku ya kumi na tatu tangu aondoke nyumbani na kuongeza kuwa ndugu walisema aliaga anaenda harusini jijini Dar, ambapo alitafutwa bila mafanikio.
Mwenyekiti akionesha eneo la kaburi alipozikwa marehemu Asha Mrisho kwa sasa.
Ilibainika kuwa marehemu kabla ya kuondoka alibadilisha kadi ya simu aliyokuwa anaitumia na kuiacha chini ya mto nyumbani kwake ambayo iligunduliwa na polisi wakati wa upekuzi.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, SACP Ulrich Matei alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
“Mpaka sasa tunawashikilia watu wawili ambao siyo wenyeji wa kijiji hicho kwa uchunguzi,” alisema Kamanda Matei.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger