MTOTO WA MIAKA 5 AKUMBWA NA GONJWA LA AJABU!

MTOTO Mariam Shabani (5) aishiye Bunju A Zone Kizota nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam  ambaye alizaliwa akiwa mzima, amekumbwa na ugonjwa wa ajabu unaowashangaza wazazi wake.
Mtoto Mariam Shabani akiwa katika mateso baada ya kupatwa na gonjwa la ajabu.
Mzazi wa mtoto huyo, Idd Shaban aliwaambia waandishi wetu kuwa mwanaye akiwa mchanga alisadikika kuwa na matatizo ya ubongo lakini ukuaji wake ulikuwa mzuri kama wanavyokuwa watoto wengine.
HALI ILIPOANZA KUBADILIKA
Akifafanua zaidi Shaban alisema: “Alipofika umri wa miaka miwili hali ilibadilika akawa mtu wa kulala tu na mpaka sasa hawezi kufanya chochote.
“Baada ya kupata hayo matatizo tuliamua kumpeleka Hospitali ya CCBRT iliyopo Msasani Dar kwa ajili ya matibabu zaidi lakini ilishindikana na madaktari walisema tuwe tunampeleka katika tawi la Hospitali ya CCBRT lililopo Tegeta kwa ajili ya mazoezi kwa ahadi kuwa hali yake itakuwa sawa.

ASHINDWA KUTEMBEA, KUONGEA
“Tuliendelea na mazoezi katika Hospitali  ya Tegeta lakini hali ilizidi kuwa mbaya kabisa kwani Mariam akawa ajiwezi kwa chochote si kutembea wala kuongea, akawa ni mtu wa kulala muda wote, mbaya zaidi mpaka sasa hawajui kama anasikia au la sababu hata tukimsemesha haonyeshi ushirikiano.

“Kwa kweli mwanangu anapata wakati mgumu sana kwani hata akiumwa hatuwezi kujua mpaka alie au awe na joto kali, kuna siku alianguka kutoka kitandani na kuvunjika mguu kiukweli tulipata tabu kumtibu kutokana na hali ya maisha kuwa ngumu, tulijitahidi akapona mguu kwa pesa za kududunduliza.
Akiwa amelala.
ALIKUWA ANAONGEA NA KUCHEKA
 “Naumia sana kuona mwanangu yupo katika hali mbaya wakati alizaliwa akiwa mzima asiye na kasoro, alikuwa anaongea, anacheka pia aliwahi kutambaa na kutembea katika ukuaji wake utotoni.
“Nakiri kuwa tuliambiwa ana mtindio wa ubongo, huenda hiyo hali ilichelewa kujitokeza mpaka baada ya miaka miwili ndipo hali hii ikajitokeza.

NATAMANI AWE AKIENDA SHULE
“Sijui hatima ya mwanangu, natamani kuona binti yangu anakwenda shule kama watoto wengine hata kama siyo shule za kawaida basi za watoto wenye mtindio wa ubongo japo uwezo kifedha sina.
“Mimi ni mjenzi na nina kipato kidogo sana, nawaomba wasamaria wema, Watanzania wenzangu wanisaidie fedha za matibabu na kibaiskeli cha kumbebea kwa sababu tumemtengenezea kiti cha mbao ambacho kinamuumiza,” alisema Shaban.

Yeyote aliyeguswa na habari ya kusikitisha ya mtoto Mariam awasiliane na mzazi wake kwa simu namba 0718 848 895.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger