Ndani ya mwezi mtukufu mastaa wengi walionekana kuvaa kiheshima huku
wakijisitiri sehemu zao nyeti lakini cha ajabu mara baada ya mfungo,
baadhi wamerejea mavazi yao ya kimitego.
Uchunguzi uliofanywa na Ijumaa mara baada ya Sikukuu ya Idd kupita
umebaini baadhi wamerejea kwenye mavazi yao ya kihasara, mazingira
yanayoashiria kuwa, walihamia kwenye mavazi ya kiheshima kinafiki.
Akizungumza na Ijumaa baada ya kumuona Wema Sepetu kwenye Uwanja wa
Ndege wa Julias Nyerere akiwa amevaa taiti nyekundu iliyobana makalio
yake, mdau mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema:
“Dah! Mwezi umeisha sasa tutakoma kwa mavazi ya kihasara, Wema
alikuwa akijisiri sana ndani ya mwezi mtukufu lakini alivyovaa leo,
daah.”
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment