skip to main |
skip to sidebar
MUME WA JACK CHUZ APATA AJALI AKIENDA KUSALI IDD
MUME wa msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack
Chuzi’, Gadner Dibibi amesherehekea Sikukuu ya Idd vibaya baada ya
kupata ajali wakati akienda msikitini.
Mume wa msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuzi’, Gadner Dibibi akionyesha majeraha baada ya ajali hiyo.
Chanzo cha habari kilitiririka kuwa, Gadner alipata ajali hiyo maeneo
ya Mlimani City alipokuwa akishuka kwenye Bajaj ambapo Bodaboda
ilimpitia na kumgonga.
Msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentezel ‘Jack Chuzi’, Gadner Dibibi wakati wa harusi yao.
“Ameumia sana, alikuwa akienda kuswali swala ya Idd lakini kwa bahati
mbaya ajali hiyo ikatokea,” alisema mtoa habari huyo aliyeomba hifadhi
ya jina lake.Gadner alipoatikana alikri kupata ajali hiyo na kueleza
kuwa, kwa sasa anaendelea kuuguza majeraha.
No comments:
Post a Comment