JINI KABULA AFUNGUKA MAZITO KUHUSU PENZI LAKE NA BUSHOKE

MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amefunguka kuwa licha ya penzi lake na msanii Maximilian Bushoke kuwa na sarakasi nyingi lakini anaamini atamuoa.
Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’
Akizungumza na paparazi wetu, Jini alisema watu wengi wamekuwa wakiuponda uhusiano wake kwa kuwa Bushoke anaishi Afrika Kusini na kuona hakuna mapenzi ya kweli lakini ukweli anaoujua yeye ndoa ipo.
Msanii wa Bongo Fleva Maximilian Bushoke.
“Piga ua garagaza, Bushoke ndiye mwanaume ambaye anajua kunipa tiba nzuri ya mapenzi, hakuna mwingine, atanioa tu kwa sababu sioni kipingamizi,” alisema Jini Kabula.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger