
Mkurugenzi Hashim Lundenga amesema “kuna kushutumiwa kwamba tunachukua rushwa ya ngono kutoka kwa Wasichana kitu ambacho sio kweli, hakuna msichana aliesema ameingia kambini au ameshinda kwa sababu ametoa rushwa ya ngono, katiba yetu inakataza kabisa yeyote kujihusisha na hilo”

.
Moja ya kesi hizo ni pamoja na ya Mchungaji aliemuondoa mwanae baada ya kupewa ubalozi wa kinywaji chenye kilevi, mrembo mwingine alikua Nadya aliekua masomoni Chuo kikuu familia yake ilikataa kabisa mtoto wao kushiriki.

.
Kwa kumalizia, Lundenga amekiri kwamba wanao utaratibu, sheria na kanuni kwenye katiba yao ambayo imepitishwa na Serikali ikiwa na maagizo mablimbali ikiwemo marufuku ya kiongozi yeyote kuomba rushwa ya ngono.
Pamoja na kuzushiwa hizo kashfa, amesema idadi ya Warembo wanaotaka kushiriki haijapungua bali imeongezeka kwa sababu Wasichana ndio wanazidi kujitokeza.
No comments:
Post a Comment