MSANII NISHA WA BONGO MOVIE AMUANIKA WAZI BWANA’KE

 Supastaa wa filamu za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’.
MSANII wa filamu anayefanya poa na muvi yake ya Zena na Betina, Salma Jabu ‘Nisha’ amemnadi bwana’ake anayejulikana kwa jina la Fahad baada ya kuweka picha kwenye ukurasa wake wa Facebook akiwa amejichora ‘Mrs Fahad.’ 
Akizungumza na mwandishi wetu, Nisha alisema kuwa hawezi kuzungumza chochote kuhusiana na mchoro huo kwa sasa lakini siku si nyingi ukweli wote atauanika hadharani. 

“Siwezi kuzungumzia chochote kuhusiana na hilo. Lakini hivi karibuni nitamtambulisha rasmi na itakuwa ‘ofisho’ watu wangu wa Global msiwe na wasi,” alisema Nisha.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger