Mwigizaji
wa kitambo kwenye tasnia ya maigizo Bongo, Augustino Mathias ‘Tino
Madhahabuna anayesumbuliwa na gonjwa baya la moyo kwa zaidi ya miaka 7.Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum juzi, mwigizaji huyo alisema kuwa mwanzoni hakujua kama ana matatizo hayo ya moyo ingawa alikuwa na dalili za ugonjwa huo.
Augustino Mathias ‘Tino Madhahabuna' akiwa ametembelewa na mwandishi wa Global publishers, Deogratius Mongela.“Ilifikia muda afya yangu ikazorota nikawa siwezi tena kufanya kazi ambazo zilikuwa zikiniingizia kipato cha kuendesha maisha kwa kuwa mimi ni baba wa watoto watano na familia yangu inanitegemea.
“Ndugu zangu kwa kweli ninateseka sana, imefikia hatua hata watu wangu wa karibu niliokuwa nikiwasaidia kwa mawazo, nao wamekuwa wananibeza kutokana na matatizo yangu ya kiafya,” alisimulia kwa majonzi makubwa na kuongeza:
Sehemu ya miguu ya msanii Augustino Mathias ‘Tino Madhahabuna' iliyovimba kutikana na ugonjwa wa moyo.“Kama wanashindwa kunisaidia kipindi hiki naumwa, wataweza kunisaidia nikifa?
“Daktari amenishauri nifanye mazoezi, amenielekeza vyakula kwa kipindi hiki, nazingatia hayo, nimekuwa naishi kwa kunyanyasika sana kama vile sina wenzangu (wasanii) hadi ndugu zangu wameamua kunisaidia kulea watoto wangu japokuwa wana maisha ya kawaida, hapa kodi na mahitaji mengine vinanisubiria.”
Kwa Mtanzania yeyote aliyeguswa na matatizo ya Tino Madhahabu anaweza kumsadia kupitia namba yake ya simu ambayo ni 0767 25 00 26 iliyosajiliwa kwa jina la Augustino Mathias. Kutoa ni moyo.

No comments:
Post a Comment