MWAKIFWAMBA: WASANII WA BONGO MUVI NO OMBAOMBA KWA SABABU WANAPENDA STAREHE

MWENYEKITI wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba amefunguka kuwa kinachowaponza wasanii wa filamu Bongo kiasi cha kuwa ombaomba ni kupenda starehe.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF), Simon Mwakifwamba.
Akichonga mbilitatu na paparazi wetu, Rais huyo alisema wasanii wamekuwa watu wa kupenda sana kupiga mitungi na kufanya starehe nyingine kwa kutumia fedha nyingi kitu kinachowapelekea kutokuwa na maendeleo katika maisha yao na kuishia kupiga mizinga tu.
“Wasanii wanapata fedha lakini cha kushangaza wanashindwa hata kujiunga na bima za afya au kuwekeza kwenye mambo muhimu, yaani mtu kutoa kiwango fulani cha fedha kwa ajili ya maisha yake ya baadaye anaona kama atamaliza fedha zake,” alisema Mwakifwamba.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger