BAADA YA KIMYA KIREFU, HATIMAYE KANUMBA THE GREAT YAKARABATIWA

BAADA ya kampuni ya marehemu Steven Kanumba, Kanumba The Great Film kudaiwa kufungwa, sasa imekarabatiwa na kuanza kazi upya.
Marehemu Steven Kanumba, Kanumba The Great enzi za uhai wake.
Mwanahabari wetu alifika kwenye ofisi hizo Jumatano iliyopita ambapo alishuhudia baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo walifanyia usafi vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuanza kazi upya.
“Tulifunga kwa muda lakini kwa sasa tumerudi kivingine baada ya kufanya maboresho katika ofisi, hivyo mashabiki wa Kanumba The Great Film wategemee makubwa,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao huku akiomba kustiriwa jina.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger