KIBANO! Staa wa sinema za Kibongo, Halima Yahya
‘Davina’ anadaiwa kupewa kipigo kikali na mumewe, muda mfupi baada ya
kukutwa akiongea kimahaba na simu iliyodaiwa kupigwa na mwanaume
mwingine.
Tukio hilo lilitokea nyumbani kwa msanii huyo, Mbezi-Beach, Dar,
Julai 22, mwaka huu ambapo Davina alikutwa akizungumza na mwanaume
ambaye haikujulikana mara moja ni nani ndipo mumewe alipomshushia kipigo
‘hevi’.
Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu familia hiyo, mume wa Davina
aliibua timbwili hilo baada ya kumsikiliza kwa makini mkewe huyo na
kugundua anazungumza na mwanaume mwingine wakiahidiana kitu f’lani.
“Mumewe alitega sikio kwa makini na kugundua alikuwa akizungumza na
mwanaume, akamsogelea karibu na kunasa mazungumzo yao, akamuoma simu
mara moja, Davina akaanza kujitetea ndipo mtiti ulipoibuka, mume akaanza
kumpiga mke ingawa hakumuumiza kiivyo,” kilisema chanzo hicho.
Baada
ya data hizo kutua kwenye Dawati la Risasi Jumamosi, mwanahabari wetu
alimvutia waya Davina ambaye alikiri kutokea kwa tukio hilo na kufafanua
kuwa hakuwa akiongea na mwanaume huyo kwa lengo baya zaidi ya maongezi
ya kikazi.
“Dah! Umejuaje hii ishu ni ya kifamilia hivyo! Mmh...kweli ninyi ni
noma, anyway ishu ni kwamba, mume wangu alinifuma nikiongea na simu ya
jamaa mmoja ambaye alikuwa ananipigia ili anipatia fedha zangu ambazo
zilibaki baada ya kufanya tangazo moja linalohusiana na mambo ya Ukimwi.
“Wakati naongea, yeye (mumewe) hakujua nini kinaendelea zaidi alikuwa
akisikia sauti ya mwanaume tu na majibu yangu kweli akajikuta amepaniki
na kunivaa akiwa ana hasira, si unajua mtu yeyote anayekupenda wivu
huwa ni kitu cha kawaida tu lakini nilimwelewesha baadaye akanielewa na
maisha yanaendele kama kawaida,” alisema Davina.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment