BABA LEVO ADAIWA KUMDUNDA SHEMEJIYE, SOMA ZAIDI HAPA

STAA wa Bongo Fleva, Trey Revocatus ‘Baba Levo’ amedaiwa kumshushia kipigo shemeji yake aliyefahamika kwa jina la Pili Kimenya, mkazi wa Kisangani, Kigoma.
Staa wa Bongo Fleva, Trey Revocatus ‘Baba Levo’ akipozi.
Kwa mujibu wa chanzo, Baba Levo alikwenda kwenye mazishi ya kaka yake ambaye alikuwa mchumba wa Pili, Patrick Revocatus, baada ya kuzika alimtuhumu shemeji yake huyo kuwa amemuibia marehemu cheni na aliposema hajachukua, jamaa akampa kipigo.
Aliulizwa Baba Levo kuhusiana na tukio hilo alisema:“Hamna mimi sikumpiga, wao na mama yake ndiyo walikuja kufanya fujo msibani nikawafungulia mashtaka polisi. Mwanamke huyo alimharibia marehemu kwa kumvutisha madawa ya kulevya.”

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger