
Kumeibuka baadhi ya jumbe fupi za
maandishi (meseji) zilizosambaa mitandaoni zikisema kuwa Dk. Wilbroad Slaa
amefariki dunia kutokana na ajali ya gari aliyoipata siku ya leo asubuhi na
mapema.
Baadhi ya meseji hizo
zilizosambaa zaidi katika mitandao ya kijamii zilisema,
"Roho ya marehemu Dk. Slaa ipumzike kwa amani”, “Bwana
ametoa na Bwana ametwaa…”. Na nyingine ziliandikwa kama habari kabisa,
“Breaking news:
Dk. Slaa hatunaye tena!
Kwa mujibu wa shirika la utangazaji la taifa (TBC) Dk. Slaa amefariki dunia
majira ya saa 3:25 asubuhi hii katika ajali mbaya ya gari iliyohusisha gari
ndogo aina ya Rav 4 na basi la abiria. Dk. Slaa na dereva wake walifariki
hapohapo.
Marehemu Dk. Slaa ameacha
mke na watoto watano. Roho ya marehemu ilale mahali pema peponi. Amina"
Taarifa kamili na ya uhakika kabisa ni kuwa Dk. Slaa ni mzima wa afya na hajapata ajali yeyote. Pia TBC haijatoa taarifa kama hiyo kwani ni uzushi tuu. Tunachowaomba ni kupuuzia taarifa hizo za uongo!
Taarifa kamili na ya uhakika kabisa ni kuwa Dk. Slaa ni mzima wa afya na hajapata ajali yeyote. Pia TBC haijatoa taarifa kama hiyo kwani ni uzushi tuu. Tunachowaomba ni kupuuzia taarifa hizo za uongo!

No comments:
Post a Comment