JOHARI AKANA KATUKATU MADAI YA KUBATIZWA

MKONGWE wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amedaiwa kubatizwa juzikati katika Kanisa Katoliki Nyalikungu wilayani Maswa, Simiyu lakini mwenyewe amekanusha.
Mkongwe wa filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’.
Chanzo makini kilichodai kushuhudia ubatizo, kilieleza kuwa Johari alifika Jumapili kanisani hapo na watu kuhoji kwa nini achelewe kubatizwa? Alipotafutwa na mwanahabari wetu, Johari alitiririka:
“Kweli nilikwenda kwenye hilo kanisa lakini sikubatizwa kama alivyosema huyo mtu. Nitabatizwaje mara mbili? Mimi nilishabatizwa tangu utotoni.”

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger