Jamani! Katika hali ya kushangaza, mastaa wa filamu
Bongo wamesusia kumbukumbu ya siku 40 ya aliyekuwa muongozaji maarufu wa
filamu nchini, George Otieno ‘Tyson’ aliyefariki dunia kwa ajali Mei
31, mwaka huu.
Shughuli ya 40 ya Tyson ilifanyika Alhamisi iliyopita nyumbani kwa
aliyekuwa mkewe, Beatrice Shayo maeneo ya Sinza-Mapambano, Dar ambapo
mastaa mbalimbali walialikwa lakini hakuonekana hata mmoja hali
iliyosababisha chakula na futari iliyokuwa imeandaliwa kubaki huku
wasanii wa vikundi waliohudhuria wakirudia mara mbilimbili.
Akizungumza na gazeti hili, Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania
(TAFF), Simon Mwakifwamba aliyekuwa kwenye shughuli hiyo alisema
anashangaa mastaa wa filamu kukacha ishu hiyo kwani alimpa taarifa
Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Nyerere’ kwamba
awaambie wahudhurie.
“Nimewaalika wasanii wote lakini hakuna aliyekuja hata mmoja, ukweli
wasanii hatuna ushirikiano kwani Tyson ndiye mwanamapinduzi aliyeigeuza
sanaa kutoka kwenye kuuza sura hadi kuwa biashara hivyo walipaswa kumpa
heshima yake,” alisema Mwakifwamba.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment