MAYA AIACHA KANUMBA THE GREAT

NDO basi tena! Staa wa sinema za Kibongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amefunguka kuwa kwa sasa amejikita katika kupiga kazi za nje ya Kampuni ya Kanumba The Great Film hivyo asiulizwe kuhusu kampuni hiyo aliyofanya nayo kazi kwa muda mrefu.
Staa wa sinema za Kibongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’.
Akichonga na mwanahabari wetu, Maya alitiririka kuwa ameamua kuiweka kando kampuni hiyo na kujikita katika kazi za nje na ikiwezekana asimame mwenyewe.
“Nipo nje ya kampuni kwa sasa, kampuni inaongozwa na mama Kanumba (Flora Mtegoa) mwenyewe, nafanya kazi na watu tofautitofauti ili baadaye nisimame mwenyewe,” alisema Maya.

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger