HAYA NDIO MANENO YA AY YA HIZI PICHA ALIZOPIGA AKIWA MAREKANI

6 
A.Y tayari ameshafika Marekani na wameanza kwa kukutana na Wafanyakazi wa ofisi ya Rais Barack Obama ambapo msafara huo wa wasanii wa Afrika umepata nafasi ya kuzunguka sehemu mbalimbali ndani ya White House ikiwemo ofisi ya Obama inayoitwa Oval.
Huu msafara wa wasanii kutoka Africa unajumuisha Femi Kuti, D Banj wa Nigeria, Victoria Kimani wa Kenya, Buffalo Soldier wa Zimbabwe na A.Y ambapo kesho wanatarajia kukutana na Rais Barack Obama.
1Baada tu ya kufika, Ay kaniambia kitu cha tofauti alichokutana nacho kwenye Ikulu hii ni kwamba jamaa wanakwenda na dress code kutokana na siku, yani imepangwa kuna mavazi ya kuvaa kutokana na siku… kwa weekend ambayo Ay na wenzake waliitembelea Ikulu mtu yeyote haruhusiwi kuvaa suti hivyo utawakuta Wafanyakazi wengine na kaptula au jeans.
Hata kina Ay wakati wanajiandaa kwenda Ikulu waliambiwa wasivae suti maana ni weekend.
2Ay anasema kingine ni kwamba Obama kila wiki anatenga siku ya kukutana na Watoto kutoka sehemu mbalimbali wanaotembelea Ikulu.
9
11
12

No comments:

Post a Comment

 
Support : WELCOME AGAIN MDADISI
Copyright © 2011. MDADISI WA MAMBO
THIS IS MDADISI
Proudly powered by Blogger