MSANII wa filamu ambaye
pia ni mweka hazina msaidizi wa klabu ya Bongo Movie Unity, Sabrina
Rupia ‘Cathy’ amefunguka kwamba anaona kundi hilo linakwenda kufa na
halitakuwepo kabisa kutokana na kujiuzulu kwa mwenyekiti wao, Steven
Mengere ‘Steve Nyerere’.
Akistorisha na paparazi wetu, Cathy alisema amejisikia vibaya Steve
Nyerere kujiuzulu na wao kama viongozi hawakuwa na taarifa hivyo
kutokana na kwamba kiongozi huyo alikuwa mpiganaji Bongo Movie itakufa
kwani hakuna mtu anayeweza kuongoza kama Steve.
“Steve yeye kama binadamu ana mapungufu kidogo lakini mazuri
aliyofanya ni mengi kwani alikuwa mpenda maendeleo lakini kujiuzulu
kwake ni pigo na ninaona kama kundi hili halitakuwepo tena, yaani
ninajisikia vibaya sana na amejiuzulu ghafla mno,” alisema Cathy.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment